• LOGIN
  • No products in the cart.

LSC: MADA KUU 1.1: WATU WA NYUMBANI

Person Milking a Cow · Free Stock Photo

Utangulizi

Je! unaishi na kina nani nyumbani? Unaweza kutamka majina yao kwa ufasaha? Kwa mfano, kuna silabi ngapi katika jina la kila mmoja wao? Mawasiliano yatakuwa kamilifu iwapo sauti, silabi na maneno ya lugha yoyote ile hutamkwa kwa namna inayostahili. Pia ni muhimu kuthamini na kushirikiana na watu wa nyumbani kimazungumzo na katika shughuli mbalimbali.

Kwa hivyo, mada hii itakupa uwezo wa kutambua matamshi bora ya sauti za Kiswahili. Mada hii pia itakuwezesha kutambua watu wa nyumbani na jinsi ya kuwasiliana na kuishi nao kwa namna inayostahili.

Funzo a: Kutamka sauti za Kiswahili
Shughuli 1.1 Kusikiliza na Kuzungumza

Katika vikundi,

1. Tamka, kariri, na kusoma kwa sauti maneno yafuatayo kwa kuzingatia matamshi bora ya vokali za Kiswahili.

a– anza, baba, kaka, dada
e– endesha, endelea,
i-inuka, ingia, bibi, mimi, sisi
o– omba, ona, ondoa, oga, wote
u– uhuru, umoja, kuku, nguvu

2. Tamka maneno yafuatayo yenye matumizi ya vokali mbili

aa– kaa, jaa, baada, saa,
ee– mzee, pekee
ii– tii, bidii
oo– choo, njoo
uu– juu, mguu

3. Tamka maneno yafuatayo yenye matumizi ya vokali mbili zisizofanana

ondoa, lia, ongea, fagia, pokea, chuo, kimbia, somea

4. Shirikiana na wenzako kutambua, kutamka na kuandika baadhi ya maneno yenye vokali mbalimbali.

Shughuli 2.1 Kusikiliza na Kuzungumza

Katika vikundi,
1. Tamka sauti zifuatazo.

i. /b/, /p/, /m/ /w/

ii. /f/, /v/

iii. /dh/, /th/

iv. /d/, /l/, /n/, /r/, /s/, /t/, /z/

v. /ch/, /j/, /ny/, /sh/, /y/

vi. /k/, /g/, /ng’/, /gh/, /kh/

vii. /h/.

2. Tamka tena sauti zilizo juu. Tambua mahali sauti hizo zinakotamkiwa.

3. Unganisha konsonanti na vokali ulizotamka hapo juu kuunda silabi na maneno.

fa, fe, fi, fo, fu

ba, be, bi, bo, bu

cha,che,chi,cho,chu

dha, dhe,dhi,dho,dhu

4. Shirikiana na wenzako katika kikundi kuandika alfabeti ya Kiswahili kutoka A hadi Z.

Funzo b. Kutambua msamiati wa watu wa nyumbani
Shughuli 3.1 Kusikiliza na kuzungumza.

Katika vikundi,

WATU WA NYUMBANI.

Majina ya ukoo;

Neno ukoo linafasiliwa kama kundi la watu wa nasaba moja. Nasaba ni uhusiano wa watuwenye uzao mmoja.

majina ya wa watu wenye uhusiano unaotokana na ukoo mmoja ni kama yafuatayo;

Baba:    Ni mzazi wa kiume au mume wa mamako.

Mama:  Ni mzazi wa kike.

Kaka:    Ni mtoto wa kiume mliyezaliwa naye.

Dada:   Ni ndugu wa kike wa kuzaliwa na nawe.

Bin :     Ni mtoto wa kiume wa mtu fulani.

Binti:    Ni mzaliwa wa kike wa wazazi.

Babu:   Ni mzazi wa kiume wa baba au mama.

Bibi/nyanya: Ni mama aliyemzaa baba au mama.

shangazi: Ni ndugu wa kike wa baba .

Ami/baba mdogo: Ni mwamume aliyezaliwa katika tumbo moja na baba.

mjomba: Mwanaume aliye ndugu wa mama au kaka wa mama.

mama mdogo: Ni mwanamke aliyezaliwa katikatumbo moja na mama.

binamu: Ni mtoto wa shangazi ami au mjomba.

Ndugu: Ni mtu wa kike au kiume aliyezaliwa naye kutoka kwa baba,kwa mama au wazazi wote wawili.

wifi:    Jina la heshima la kifamilia waitanaklo mke na ndugu wa kike wa mume.

shemeji : Ni ndugu au rafiki wa mke au mume.

mkwe:    Ni baba au mama wa mume au mke wako .aidha ni mume au mke wa mwana wako au binti yako.

mama mkwe: Ni mama wa mkeo au mumeo.

baba mkwe/bamkwe: Ni mzazi wa kiume wa mke au mume wa mtu fulani.

2. Jadiliana na wenzako kutafuta maana ya maneno uliyopewa katika boksi


3. Elezea kuhusu watu wa familia yako kwa kutaja majina yao.

4. Shirikiana na wenzako kusoma na kujadili maana ya sentensi zifuatazo

i. Baba yangu ni dereva wa basi.

ii. Mama yangu ni mwalimu wa Kiswahili.

iii. Dada yake Peter anafundisha katika Chuo Kikuu cha Kyambogo.

iv. Bin yangu anaitwa Haba.

v. Kaka yangu anasomea katika Chuo cha walimu cha Nakaseke.

vi. Binti yake Yusuph ni mrembo sana.

vii. Tafadhali niitie yule kaka yangu.

viii. Eve ni binti yake mzee Lutaaya.

ix. Dada yako anaitwa nani?

x. Mama ananyonyesha mtoto.

Kazi mradi
Katika kikundi, fanya utafiti kuhusu msamiati mwingine wa watu wa ukoo. Unaweza kutumia kamusi, maktaba au mtandao. Kisha, wasilisha matokeo ya utafiti wako darasani.

5. Ambatanisha majina ya watu wa ukoo kutoka sehemu A na B.

A                                                               B

Baba                                                  ndugu wa kike wa baba.

Mama                                                mzazi wa kiume.

Shangazi                                            ndugu wa kike wa kuzaliwa na kaka.

Kaka                                                   mzazi wa kike.

Dada                                                   ndugu wa kiume wa kuzaliwa na dada.

Nyanya                                              mzazi wa kike wa baba au mama.

Funzo c: Kuigiza majukumu ya watu wa Nyumbani
Shughuli 4.1 Kusikiliza, Kuzungumza, Kusoma na Kuandika

Baba anakama ng’ombe.                                        Mama anapika chakula.

Milking a cow hi-res stock photography and images - AlamyThe Cooking Mom Gift Guide

Dada anaosha vyombo.                                   Kaka anafyeka nyasi.

6,159 Woman Washing Dishes Photos and Premium High Res ...Sprucing up our School before Exams! | Family Care Uganda

3. Shirikiana katika vikundi kuelezea na kuigiza majukumu mbalimbali ya watu wa nyumbani.

Funzo d. Kueleza kazi zinazofanyika nyumbani
Shughuli 5.1 Kusikiliza, kuzungumza na kuandika

Katika vikundi,

1. Jadiliana kuhusu kazi mbalimbali zinazofanyika nyumbani kwenu.
2. Kwa zamu, elezea kazi unazofanya nyumbani kwenu wakati wa likizo.
3. Jaza mapengo kwa kutumia vitenzi vifuatavyo vinavyohusu kazi za nyumbani.

(paka, ezeka, jenga, safisha, fyeka)

(a) Dada yangu ana ………………… vyombo.
(b) Ami ali ………………… nyasi katika boma lake.
(c) Baba yetu anafanya kazi ya ku ………… rangi.
(d) Nili ………… mabati juu ya nyumba yetu.
(e) Babu yetu ali …………. nyumba kubwa sana kijijini.

Funzo e. Kusimulia hadithi fupi kuhusu familia
Shughuli 6.1 Kusikiliza, kuzungumza na Kuandika

Chora watu unaoishi nao nyumbani kwenye karatasi, kisha usimulie hadithi inayohusu watu wa familia yako.

Funzo f. Kutambua matumizi ya Salamu na maneno ya adabu
Shughuli 7.1 Kusikiliza na kuzungumza.

Taz: Salamu ni maamkizi ya kujuliana hali miongoni mwa watu. Katika lugha ya Kiswahili kuna aina nyingi za salamu kulingana na umri/cheo, wakati, hali, idadi ya watu unaosalimia na uhusiano wa watu husika.

Salamu kulingana umri/cheo: Shikamoo ni salamu ya heshima kwa mtu anayekuzidi umri au cheo.

 watoto wanamsalamia mke.

Students Pay Respect To Teachers Vector Design Stock Vector - Illustration  of child, woman: 213446599

salamu kulingana na wakati.

salamu                    jibu

sabalkheri              sabalkheri/alkheri

masalkheri             masalkheri/alkheri

TANBIHI:Sabalkheri ni salamu inayotumiwa wakati wa asubuhi ilihali masalkheri inatumiwa wakati wa jioni kuanzia alasiri

 Salamu kulingana na hali mbalimbali

    Salamu                                           Hali                                                  Jibu

habari ya /za                                  masomo/shuleni?                               nzuri/njema.

habari ya/za                                   nyumbani?                                          nzuri/njema

habari ya/za                                   safari?                                                  nzuri/njema

habari ya/za                                   kupotea?                                              nzuri/njema

habari ya/za                                   kazi?                                                     nzuri/njema

      iii. Salamu za kujuliana hali kulingana na idadi ya wanaoitikia.

Shughuli 8.1 Kusikiliza na kuzungumza

Kakika vikundi,

1. Igizeni salamu na majibu yake kama ifuatavyo;

   Salamu                                                   Jibu

hujambo?                                                Sijambo.

hamjambo?                                             Hatujambo.

umeamkaje/umelalaje?                           Salama.

mmeamkaje/mmelalaje?                         Salama.

umeshindaje?/mmeshindaje?                  Vizuri/vyema.

u mzima? m wamzima?                            Ni mzima/ tu wazima.

u hali gani?/mhali gani?                           Njema/nzuri.

Funzo g. Kutambua na kuigiza maneno ya adabu

Shughuli 9.1 Kusikiliza, kuzungumza na kusoma

Katika vikundi,

Funzo h. Kusoma na kuigiza mazungumzo
Shughuli 10.1 Kusoma na kuandika

1. Katika jozi, someni na kuigiza mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali

Tom : Habari ya siku nyingi rafiki?
Rehema : Ni nzuri, labda zako?
Tom : Mimi ni mzima. Umepotea sana siku hizi!
Rehema : Ndiyo, mama yangu amekuwa mgonjwa.
Tom : Eee! Pole sana, sasa yuko vipi?
Rehema : Tumempa dawa, atapata nafuu.
Tom : Hebu tuombe Mungu apone haraka
Rehema : Amina. Hebu niende nyumbani, Alamsiki!

i. Kwa kutumia kamusi, tafuteni maana ya maneno mapya kutokana na mazungumzo.
ii. Tambua na kuandika salamu na maneno ya adabu yaliyotumika katika mazungumzo.

Sarufi
Funzo i. Kutumia vipatanishi sahihi vya nomino za ngeli ya A-WA katika sentensi
Shughuli 11.1 Kusoma na kuandika

Katika vikundi,

1. Tazameni na kujadiliana kuhusu kinachotendeka katika michoro.

Ngeli ya A-WA inajumuisha viumbe wote wenyeuhai na damu kama vile watu,wanyama,wadudu, ndege nakadhalika.

Shirikiana kusoma kwa sauti na kutafuta maana ya nomino zifuatazo;

    Umoja                                             Wingi

mtu                                                            watu

mtoto                                                        watoto

mhubiri                                                      wahubiri

mke                                                            wake

mume                                                         waume

mkulima                                                      wakulima

mzazi                                                           wazazi

mwalimu                                                      walimu

mfalme                                                        wafalme

mwanafunzi                                                 wanafunzi

mlevi                                                            walevi

mlinzi                                                           walinzi

mwislamu                                                    waisilamu

msichana                                                    wasichana

mvulana                                                     wavulana

UPATANISHO WA KISARUFI

A(UMOJA)

majina             vionyeshi        kuwa      vivumishi

mtu                 huyu                 ni             mrefu

mgeni              yule                  si             mfupi

mdudu                                                     mbaya

mnyama                                                   mdogo

1, mtu huyu ni mrefu.

2,mtoto yule si mbaya.

3, mdudu yule ni mbaya.

B ,(WINGI)

majina             vionyeshi       kuwa         vivumishi

watu                 hawa            ni                warefu

wageni              wale            si                  wafupi

wadudu                                                    wabaya

wanyama                                                  wadogo

1,watu hawa ni warefu.

2,watoto wale si wabaya.

3,wadudu wale ni wabaya.

majina (umoja)                      vimilikishi

mzazi                                       wangu(my /mine)

mpishi                                      wako(your/s)

mgeni                                       wake(his /her)

mgonjwa                                  wetu(our/s)

wenu(their)

wao(your /p)

1,Mzazi wangu ni mzuri.        Wazazi wangu ni wazuri.

2,Mtoto wangu ni mbaya.      Watoto wangu ni wabaya.

3,Mpishi wako ni msafi.         Wapishi wako ni wasafi.

4,Baba yangu ni mrefu.         Baba zangu ni warefu.

5,Binti yake ni mkubwa.        Binti zake ni wakubwa.

majina                       kiwakilishi(a-)                               kiwakilishi(wa-)

msichana                    anasoma                                      wanasoma

mwalimu                    analala                                          wanalala

mnyama                     anakula                                         wanakula

mganga                     anakimbia                                      wanakimbia

1, Msichana anasoma.        Wasichana wanasoma.

2,Mwalimu analala.             Walimu wanalala.

3,Mnyama anakula.              Wanyama wanakula.

Shirikiana na wenzako kuandika sentensi zifuatazo katika wingi.
i. Mama analima shambani.
ii. Kaka na dada wanaosha vyombo.
iii. Mfalme amekaa.
iv. Mganga anatibu mgonjwa.
v. Mvulana anapasua kuni.
vi. Mzee anapeana mawaidha.
vii. Mwanafunzi alienda shuleni asubuhi.

Funzo j. Kuakifisha kwa usahihi
Shughuli 12. 1 Kusoma na kuandika

Katika vikundi,
1. Someni na kujadili ujumbe katika kifungu.

Nalubega na Onyango ni marafiki sana. Siku moja, Nilimsikia Onyango akisema, “Mimi na rafiki yangu Nalubega tumetembelea mataifa mengi ulimwenguni.” Kwa mfano, Mataifa ya Afrika Mashariki (Kenya, Tanzania, Sudani Kusini, Rwanda na Burundi), Ujerumani, Uhispania, Brazil, Marekani na Uchina. “Umetembelea nchi gani wewe?” Aliniuliza. “Mimi sijawahi hata kuvuka mpaka wa Uganda!” Nilimjibu. Alaa! Alishangaa. Bahati yako itakuja usijali. Alinitia moyo.

2. Tambua na kuandika alama za uakifishaji katika kifungu ulichosoma.

3. Fanyeni utafiti kuhusu alama nyingine zozote za uakifishaji ambazo hazijatajwa katika kifungu.

Funzo K. Kuandika Insha
Shughuli 13.1 Kuandika

Katika makundi,

1. Andikeni insha kuhusu watu wa ukoo wako.
Zingatieni yafuayo;
Jina lako? Unasoma kidato gani? Unaishi wapi? Unaishi na nani nyumbani? Watu wa nyumbani kwenu wanafanya kazi gani? Wewe, unasaidiaje wazazi wako katika kazi za nyumbani.

Shughuli ya jumla

Umeandaliwa sherehe ya siku ya kuzaliwa kwako nyumbani kwenu. Umeita baadhi ya
marafiki zako kutoka darasani mwako kuhudhuria. Baada ya chakula na kukata keki,
umeombwa kutambulisha kila mtu aliyehudhuria. Umemaliza kuwatambulisha marafiki
zako.
a. Watambulishe watu wa ukoo wako waliohudhuria.
b. Kila mtu wa nyumbani alisema kuwa marafiki zako ni watoto wenye adabu. Ni mambo gani waliyofanya ili kuonyesha kuwa ni wenye adabu.
c. Andika maneno uliyozungumza wakati wa hotuba yako.

Muhtasari wa mada
Katika mada hii, umejifunza kuhusu,

• Sauti za Kiswahili kwa usahihi
• Msamiati wa watu wa nyumbani.
• Usimulizi w hadithi fupi kuhusu familia yako.
• Salamu kwa namna inayostahili.
• Maneno ya adabu
• Uigizaji wa mazungumzo.
• Matumizi ya aina mbalimbali ya majina ya watu wa nyumbani katika sentensi.
• Vipatanishi vya nomino vya ngeli ya A–WA katika sentensi.
• Uakifishaji.
• Uandishi wa insha

 

Courses

Featured Downloads