• LOGIN
  • No products in the cart.

LSC: MADA KUU 1.6: BIASHARA

LSC: MADA KUU 1.6: BIASHARA

Uganda Currency - Uganda Tours | Safaris Uganda  Uganda Currency: 12 Things to Know (Money, Shillings, and Costs) |  Storyteller Travel

Utangulizi

Kila mtu, kwa njia moja au nyingine, ameshiriki katika biashara. Amefanya hivi kwa kuuza au kununua kitu kutoka mahali fulani. Je, wewe umewahi kuuza au kununua kitu? Ikiwa jibu lako ni ndiyo, ulikinunua kutoka wapi; dukani, sokoni au kutoka kwa mtu? Mada hii itakufunza msamiati unaotumia katika biashara na jinsi utakavyoutumia kujinufaisha wewe mwenyewe.

Funzo a: Kutambua msamiati wa bidhaa za dukani na sokoni

Shughuli 1.6: Kusikiliza na kuzungumza

Katika makundi,

1. Jadiliana kuhusu msamiati ufuatao na kisha;
i. Elezea maana ya kila msamiati
ii. Tumia msamiati huo kutunga sentensi kimapokezi

chumvi       mtama      mkate

kabichi       mawele     mteja

sukari         bidhaa      bei

mchele       ngano       nyanya

wimbi         vibiriti        nyama

2. (i) Tajeni bidhaa tano zinazopatikana katika duka lililokaribu na nyumbani kwenu.
(i) Je, soko lililokaribu na kwenu linauza nini? Toa mifano mitano.

Funzo b: Kutunga sentensi kwa kutumia msamiati unaohusiana na ununuzi na uuzaji wa bidhaa

Shughuli 2.6: Kusoma na kuandika

Katika vikundi,

i. Shirikiana na kujadili msamiati unaohusiana na ununuzi na uuzaji wa bidhaa na kisha, tumieni msamiati huo kutunga sentensi.
ii. Kila kikundi kisome kwa usahihi na kutunga sentensi sahihi kwa kutumia msamiati ufuatao:

pesa  deni  hasara   mtaji  nunua  hisa  bima

salio  faida  mteja  bidhaa  uza   kipato  bei  fedha .

Funzo c: Kuigiza mazungumzo kati ya mnunuzi na muuzaji

Shughuli 3.6: Kusikiliza na kuzungumza

Katika jozi,

Igizeni mazungumzo kwa zamu kati ya muuzaji na mnunuzi. Kila mzungumzaji azungumze angalau mara sita.

Funzo d: Kusoma Makala kuhusu shughuli za kibiashara

Shughuli 4.6: Kusoma

Katika vikundi,

i. Someni kimya makala ifuatayo, na kisha mjadiliane ujumbe uliomo katika Makala.
ii. Someni kwa sauti makala ifuatayo na kuelezea ujumbe uliomo
iii. Kila kikundi kijibu maswali yanayopatikana mwishoni mwa makala.

Katika maisha ya binadamu soko ni sehemu nyeti sana kibinafsi, kijamii na kitaifa.

Mwanadamu ana mahitaji mengi sana katika kukimu maisha yake na miongoni mwa hayo kubwa ni chakula.

Hatua ya mwanzo imesimamia kilimo na hata wahenga walisema kuwa ‘Kilimo ni uti wa mgongo wa maisha’. Kwa maana hiyo bila ya kilimo, maisha ya binadamu yamo mashakani. Pia, bila ya harakati za kilimo, soko halitapatikana kwani bidhaa za sokoni tuzitumiazo zatokana na kilimo. Kwa mfano nguo ni pamba, mbao ni miti na vinginevyo.

Wakulima wengi na wasiokuwa wakulima tegemeo lao kubwa ni soko. Bali si hao tu. Taifa nalo linategemea soko. Mkulima hulima akachukua mazao ya mimea sokoni akauza ili apate fedha. Asiyekuwa mkulima pia shamba lake ni soko na ndio maana wajuzi wa kusema huamba eti soko ni shamba la wavivu. Kwa vile ulimwengu wa siku hizi jinsi ulivyoendelea umetenga maeneo maalum ya kuendesha shughuli kama hizo za uuzaji na ununuaji wa bidhaa za sokoni. Na hapo ndipo pia taifa hupata pato lake kwa kupitia serikali za mitaa kuwatoza ushuru wale washiriki wa biashara zinazofanywa sokoni.

Maswali:

1. Ipe makala hii kichwa mwafaka.
2. Kwa nini soko ni sehemu nyeti sana katika maisha ya binadamu?
3. Bidhaa nyingi za sokoni zinatokana na nini?
4. Taja bidhaa zinazotokana na ukilima/ kilimo.
5. Ni nini tegemeo kubwa la wakulima?

Sarufi

Funzo e: Kutambua nomino za ngeli ya i-zi na kuzitumia kutunga sentensi kwa kuzingatia vipatanishi vya ngeli ya i-zi

Shughuli 5.6: Kusikiliza, Kuzungumza, Kusoma na kuandika

Katika vikundi,

1. Shirikiana kutambua nomino za ngeli ya i-zi kwa umoja na wingi na kisha kila mwanafunzi aziandike katika daftari lake.
2. Shirikiana pia kutunga sentensi sahihi kwa kutumia nomino za ngeli ya i-zi kwa umoja na wingi.

NGELI YA “I-ZI”

Nomino katika ngeli hii huanza kwa kiambishi “ n” katika umoja na wingi. Hii ndiyo sababu ngeli hii imekuwa ikijulikana kuna ngeli  ya “N” kwa sarufi ya kimapokeo.

UMOJA                                   WINGI

Nyumba                         nyumba

nguzo                             nguzo

njugu                             njugu

ngazi                             ngazi

ndizi                              ndizi

ndoo                           ndoo

nyama

nyota

njia

nafasi

nyika

nta

ndoa

ndoto

njaa

njuga

Nomino zifuatazo pia zimo katika ngeli ya (i-zi) ingawa hazianzi kwa kiambishi N kwa vile herufi kutangulia herufi ambazo nomino hizo huanza nazo.

kamusi  damu  mvua  chumvi  tufani   alama tauni

pombe  firimbi  siri  sahani risasi  meza  pombe

sukari    siri   pamba   bahari   adabu  adhabu

faida   barabara  chuki  mbiu  fedha  biblia

Majina vionyeshi kuwa vivumishi
Nyumba

Nyota

Mbegu

Hii

ile

Ni

Si

Nzuri

Ndogo

Ndefu

Ngumu

  A,UMOJA

 

  B,WINGI

MAJINA VIONYESHI KUWA VIVUMISHI
Nyumba

Nyota

Mbegu

hizi

zile

 

ni

si

Nzuri

Ndefu

Ndogo

Ngumu

 

C

UMOJA WINGI
MAJINA                                   VIMILIKISHI

Nyumba                                yangu

Nyota                                     yako

Mbegu                                   yake

Taa                                          yetu

Amri                                       yenu

Kazi                                         yao

 

 

MAJINA                    VIVUMISHI

Nyumba                   zangu

Nyota                       zako

Mbegu                      zake

Taa                           zetu

Amri                       zenu

Kazi                         zao

UMOJA WINGI
MAJINA                                    KIWAKILISHI

Nyumba                                                                                     imeanguka

Suruali                          imeibwa

Nguo                           imeletwa

Sahani                         imepotea

Kazi                            imekwisha

Likizo                                        imependeza

Meli                      imefika

 

MAJINA                                                  KIWAKILISHI

Nyumba                                zimeanguka

Suruali                                       zimeibwa

Nguo                                          zimeletwa

Sahani                                      zimekwisha

Kazi                                            zimepotea

Likizo                                       zimependeza

 

Funzo f: Kutunga sentensi kwa kutumia nyakati mahsusi

Shughuli 6.6: Kusikiliza, Kuzungumza, Kusoma na Kuandika

Katika vikundi,

Kumbushana msamiati wa biashara ulioko katika ngeli ya i-zi na kuutumia kutunga sentensi sahihi. Sentensi zitungwe kwa umoja na wingi kwa kutumia njeo zifuatazo: na, ta, li, me.

Funzo g: Kuandika insha juu ya bajeti ya shilingi 10,000 utakazotumia

Shughuli 7.6: Kuandika

Katika vikundi,

Jadiliana kuhusu jinsi utakavyotumia shilingi elfu kumi. Baada ya majadiliano, tungeni insha juu bajeti ya shilingi elfu kumi au kiasi chochote cha pesa. Insha ya kila kikundi iwekwe kwenye chati na kutundikwa ukutani ili wanavikundi vingine waione.

Taz: Sarafu ni vipande vya fedha, karatasi au shaba vinavyothaminiwa na kutumiwa kama pesa za nchi husika.

SARAFU TAIFA/NCHI
Shillingi Uganda/Tanzania/Kenya
Dola Marekani
Pauni Uingereza
Faranga Ufaransa /ubelgiji /rwanda
Dinari Nchi za mashariki ya kati

Shughuli ya Jumla

Wazazi wako wamekupa shilingi 50,000 kwenda kununua vitu kutoka sokoni. Vitu utakavyonunua ni vya kutumia wakati wa sherehe ya kuzaliwa kwa dada yako ambako kutakuwako wiki ijayo.

a. Taja majina ya vitu ambavyo utanunua ili kuvitumia katika sherehe hiyo.

b. Kwa kila kitu ulichonunua, tumia jina la kitu hicho kutunga sentensi kwa umoja na wingi.

c. Simulia hadithi kuhusu jinsi ulivyotoka nyumbani kwenda sokoni, vitu ulivyonunua na namna ulivyorudi nyumbani.

d. Chagua Rafiki yako humo darasani na muigize mazungumzo; wewe ni mnunuzi na yeye ni muuzaji.

Muhtasari wa mada

Katika mada hii, umejifunza kuhusu

a. kutambua misamiati ya sarafu mbalimbali.
b. kutambua misamiati ya bidhaa za dukani na sokoni.
c. kabaini misamiati ya ununuzi na uuzaji wa bidhaa.
d. kuigiza mazungumzo ya ununuzi na uuzaji wa bidhaa.
e. kusoma makala yanayohusu shughuli za kibiashara.
f. kutambua matumizi ya upatanishi wa kisarufi wa ngeli ya I–ZI.
g. kutambua vivumishi vya a-unganifu na matumizi yake katika sentensi.
h. kueleza matumizi ya vielezi husika katika sentensi.
i. kuandika insha ya mwongozo ya bajeti kuhusu vile utatumia shilingi 10,000/=.

 

Courses

Featured Downloads